Watu 8 wameuawa serikali yatoa amri ya kutotoka nje Nakuru

  • 6 years ago

Awamu ya pili ya ufurusho wa Msitu wa Mau utaendelea licha ya mapigano ambayo yameshuhudia baina ya jamii tofauti maeneo ya Narok na Nakuru. Waziri wa Mazingira, Keriako Tobiko anasema wanaochochea jamii kupigana ili kuhujumu uhifadhi wa msitu huo wanafaa kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria

hayo yanajiri huku utulivu ukishuhudiwa katika eneo la Neissut, Njoro kaunty ya Nakuru, eneo ambalo vita dhidi ya jamii mbili imesababisha mauwaji ya watu nane na kutiwa ndani kwa zaidi ya watu kumi na moja.